Home Music Diamond Platnumz Ft Tanzania All Stars – Lala Salama Magufuli

Diamond Platnumz Ft Tanzania All Stars – Lala Salama Magufuli [Mp3 Download]

3,395
Diamond Ft Tanzania All Stars – Lala Salama Magufuli
  • Diamond Platnumz Ft Christina Shusho , Jux , Mbosso , Joel Lwaga , Marioo , Zuchu , Darassa , Barnaba , Maua Sama , Ben Pol , Lava Lava , Khadija Kopa , Malkia Karen , Dulla Makabila , Queen Darleen , Baba Levo , G Nako , Cyrill Kamikaze , Mrisho Mpoto , Chege , Rayvanny , Madee , Belle 9, Maarifa & Abby Chams – Lala Salama Magufuli.

    Wasafi Media presents to you a brand new song tagged as a tribute song dedicated to the late and former president of The republic united of Tanzania John Pombe Magufuli.

    RELATED: Diamond Platnumz – Super Woman Ft Tanzanian Men All Star

    This song features all top Bongo Fleva and Hip Hop artists in Tanzania including; Diamond Platnumz Ft Christina Shusho , Jux , Mbosso , Joel Lwaga , Marioo , Zuchu , Darassa , Barnaba , Maua Sama , Ben Pol , Lava Lava , Khadija Kopa , Malkia Karen , Dulla Makabila , Queen Darleen , Baba Levo , G Nako , Cyrill Kamikaze , Mrisho Mpoto , Chege , Rayvanny , Madee , Belle 9, Maarifa & Abby Chams

    RELATED: Zuchu – Tanzania Ya Sasa (Prod. Lizer)

    Apart from being the president of Tanzania Late Magufuli served as Minister of Works, Transport and Communications from 2000 to 2005 and 2010 to 2015 and was chairman of the Southern African Development Community from 2019 to 2020.

    Similar songs dedicated to Late Magufuli

    Lyrics

    [Mbosso]

    Nalifuta chozi kushoto
    Kulia latiririka
    Maumivu moyo wa moto
    Nafsi yatatarika

    Vilio wakubwa watoto
    Iyoo we zinasikikika
    Wachonge zetu changamoto
    Wapi zitashikika

    [Christina Shusho]
    Umelala iyoo, baba umelala wee
    Nenda we Magufuli nenda wee
    Tulikupenda Mungu kakupenda zaidi
    Baba nenda wee, baba nenda wee

     

    [Jux]
    Yaani baba (Baba)
    Tutakukumbuka kwa mazuri yako
    Sema baba (Baba)
    Tutakukumbuka kwa upendo wako

    [Madee]
    Kuna Muda nalega nakosa power
    Nasema no God hii sio sawa
    Mbona kuna wengi tu walipaswa kwenda
    Unajibu “NO” huyu niliyempenda

    Umempenda John, umemchukua john
    Umetuacha hatuoni sio alfajiri sio jioni
    Tukifikicha mboni kule mbele hatuoni
    Mungu akulaze baba mahali pema peponi

    [Joel Lwaga & Diamond Platnumz]
    Kweli vyema havidumu
    Ni machozi na uchungu
    Ni ghafla, ni ghafla
    Asante kwa kujenga Tanzania imara
    Nenda, nenda, nenda ulale

    Ulale salama, pumzika baba
    Ulale salama, kazi umeifanya
    Ulale salama, tutakuenzi daima
    Ulale salama

    [Zuchu]
    Huzuni imetawala
    Jembe Tanzania limetutoka
    Yaani kama masihara leo taifa tunahuzunika
    Baba uende salama, tutakukumbuka sana
    Akupake Maaulana Amina

    []
    Miundo mbinu tunaona (Ona)
    Elimu bure tunasoma (Soma)
    Makao makuu kwetu Dodoma
    Umetupa heshima baba

    [Khadija Kopa]
    Eti njia yetu ni moja
    Umetanguli si tunafuatia
    Tunajikongoja taifa laumia
    Tunakulilia

    [Baba Levo]
    Kiumbe jasiri tena mahiri
    Ametutoka (Ametutuka)
    Jasiri mwenye akili
    Ametutoka (Ametutoka)
    Magufuli wewe ameondoka
    Simanzi Tanzania ametutoka

    [Mrisho Mpoto]
    Ina maana mapambano kikomo ndio imefikia
    Vuta nikuvute historia inakwenda kubakia
    Kila ulimi kifafa umeshikwa
    Hauwezi kusema hauwezi kuteta
    Daima ulisema tukuombee
    Ah, ila mauti yamevikwa taji dhidi ya dua
    Daima tutakukumbuka

    [Rayvanny]
    Jioni jua limezama
    Umetangulia ulale salama
    Kila ulosema limetimia
    Serikali Dodoma imehamia
    Baba mbona hujasubiria
    Ikulu ulojenga mwenyewe hujaingia

    Ulale, ulale salama
    Ulale salama, ulale salama
    Ula ula ulale, ulale salama
    Ulale salama (Ulale baba)

    Lala, lala
    Lala lala
    Lala lala

    [G Nako]
    Kilio ukiskie kwa jirani
    Machozi machozi nani afute nani?
    Kifo kifo, kifo kifo
    Kifo fumbo kubwa duniani

    [Lava Lava]
    Ni mengi ulituhusia
    Upendo mimi na yule
    Elimu bora ukatupatia
    Watoto waende shule

    Tuchape kazi ukasisitizia
    Tusikae bure
    Mbona sasa umetukimbia
    Umetuacha na simanzi baba

    [Darassa]
    Mungu ana njia zake huwezi hata kumuotea
    Mungu anachukua hata unachokinyenyekea
    Unachotegemea nguzo yako kuegemea
    Ndio maana dini zinasema tuishi kwa ku prepare

    Look alas, now we breathe like there is no air
    Should I continue singing?
    Or let me pray for better days to come
    Rest in Peace uncle Magu till we meet again Amen

    []
    Umetutoa kwenye sifuri mpaka uchumi wa kati
    Madaraja babara nzuri ona mwendo kasi

    [Khadija Kopa]
    Wanawake umetusimamia
    Kwenye sekta mbalimbali
    Umetusimamisha umetuinua

    Ulivyomteua Samia
    Umetupa ujasiri tupambane
    Asante Magufuli

    []
    Kila saa uliimaliza migogoro
    Njoo uuzindue mradi wako Morogoro
    Baba (Baba) Baba (Baba)

    Hivi sivyo tulivyotegemea
    Imeanguka nguzo tuloegemea
    Baba (Baba) Baba (Baba)

    Ulale Salama
    Ulale salama, ulale salama
    Asante kwa wema wako
    Ulale salama, asante kwa wema wako
    Ulale salama

    [Queen Darleen]
    Matibabu bure kwa watoto na wazee
    Hukutuacha nyuma wanawake twendelee

    [Marioo]
    Atufute nani machozi
    Taifa lakulilia
    Atatuvusha nani mwokozi
    Na nahodha umetangulia

    Yametutawala majonzi
    Baba umetukimbia
    Zimetushafura pozi
    Huzuni imetuelemea baba

    [Abby Chams]
    Nuru yaangaza taifa
    Imekatizwa ghafla
    Magufuli baba yetu
    Tutakukumbuka daima

    Pumzika kwa amani
    Is out of faith —
    All have left is memories
    And — let go

    []
    Hukuwa Mungu tujue umetimia
    Singeshindwa ubaki wewe
    Ili achukue vichaa mia
    Ila kama ambavyo mwewe hachagui kuku
    Maiti hachagui sanda na kifo hakichagui mtu

    [Barnaba Classic]
    Kina mama wenye hali za chini
    Bodaboda hali za chini
    Raia hali za chini
    Wanakuita Magufuli simama

    Najihisi kukata tamaa
    Ila inanibidi nikubali
    Ila Magufuli simama

    Ni mengi uliyotenda kwa ushujaa
    Haitoshi ulikuwa mzalendo
    Magufuli simama
    Uliipigania haki hukubagua watu wala mtu
    Magufuli simama

    []
    Mkombozi wa wanyonge umeenda (Aah umeenda)
    Jasiri mtenda haki umeenda (Aah umeenda)
    Kipenzi cha wananchi umeenda (Aah umeenda)
    Mpenda maendeleo umeenda (Aah)

    [Chege]
    Baba ulale salama, ulale salama
    Daddy ulale salama, ulale salama
    Hivi kweli tutacheza tena, ulale salama, ulale salama
    Uuu la, ulale salama, ulale salama

    [Cyril Kamikaze]
    Kiongozi jasiri ambaye alipinga rushwa
    Alinyanyua wanyonge pale tu alipoangushwa
    Hakuogopa fisadi yeyote yeye alimgusa
    Huduma kwa wakati bila hata kuzungushwa
    Ona barabara vijijini tunafika
    Pumzika peponi chuma daima utakumbukwa
    Ulale salama, uuuuu..

    [Diamond Platnumz & Tanzania All Stars]
    Ulale salama, ulale salama
    Ulale salama, ulale salama
    Ulale salama, ulale salama
    Ulale salama, ulale salama

    Ulale salama, ulale salama
    Ulale salama, ulale salama
    Ulale salama, ulale salama
    Ulale salama, ulale salama